Magazeti leo Desemba 26,2025

RAIS wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni amezindua rasmi Uwanja wa Hoima City wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000, sehemu ya maandalizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, litakaloandaliwa kwa pamoja na Uganda, Kenya na Tanzania.
Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Museveni alisema maendeleo yanayoendelea nchini Uganda ni matokeo ya sera za kimapinduzi, akitolea mfano mafanikio ya kampuni ya Kira EV inayotengeneza mabasi ya umeme, ambayo tayari imepokea oda ya mabasi 450 hadi Afrika Kusini.

Rais pia alisema Uwanja wa Hoima City ni mojawapo ya miradi 10 ya kimkakati inayotekelezwa kwa ajili ya maandalizi ya AFCON 2027, akipongeza kampuni ya Kituruki Summa kwa kazi nzuri ya ujenzi na kuahidi kuendeleza ushirikiano katika miradi mingine ya maendeleo.










Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news