Magazeti leo Desemba 28,2025

Katibu wa Kamati ya Mapinduzi Cup, Rashid Said Suleiman, amesema kuwa moja ya vigezo muhimu kwa timu kushiriki Michuano ya Kombe la Mapinduzi ni lazima iwe timu ya Ligi Kuu, hususan kutoka Tanzania Bara au Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari Desemba 27, 2025, kuelekea ufunguzi wa Michuano ya Kombe la Mapinduzi 2026 utakaofanyika katika Uwanja wa Amaan New Complex, jijini Zanzibar, Suleiman amesema kuwa mbali na mshindi kupewa Kombe la Mapinduzi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, atatoa zawadi ya fedha kwa mshindi wa kila mechi kupitia Mfuko wa Rais wa Zanzibar.

Aidha, jumla ya klabu 10 zimepangwa kushiriki michuano hiyo ya msimu huu, ambapo zimegawanywa katika makundi matatu. Kundi A linajumuisha Mlandege, Azam FC, Singida Black Stars na URA ya Uganda. Kundi B lina Simba, Mwembe Makumbi na Fufuni, huku Kundi C likiwa na Yanga, TRA United na KVZ.

Michuano ya Kombe la Mapinduzi msimu huu inatarajiwa kuanza Jumapili na itafikia tamati Januari 13, 2026, siku moja baada ya maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika Januari 12,1964.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news