Magazeti leo Desemba 29,2025

BODI ya Maji Bonde la Rufiji kupitia Mradi wa NBS–USANGU imeanza rasmi zoezi la urejeshaji wa mito iliyokuwa imepoteza uelekeo wake wa asili au kukauka kabisa kutokana na kujaa mchanga, hali iliyosababisha changamoto kubwa kwa wananchi na kuathiri uzalishaji wa kilimo katika Bonde la Usangu.
Akizungumza baada ya ziara ya Kamati ya Uongozi wa Mradi iliyotembelea eneo la urejeshaji wa Mto Mlowo, Mkurugenzi wa Bodi hiyo, Mhandisi David Munkyala, alisema mradi huo ni hatua muhimu katika kulinda rasilimali za maji na kurejesha ikolojia ya mito kwa manufaa ya wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news