BODI ya Maji Bonde la Rufiji kupitia Mradi wa NBS–USANGU imeanza rasmi zoezi la urejeshaji wa mito iliyokuwa imepoteza uelekeo wake wa asili au kukauka kabisa kutokana na kujaa mchanga, hali iliyosababisha changamoto kubwa kwa wananchi na kuathiri uzalishaji wa kilimo katika Bonde la Usangu.
Akizungumza baada ya ziara ya Kamati ya Uongozi wa Mradi iliyotembelea eneo la urejeshaji wa Mto Mlowo, Mkurugenzi wa Bodi hiyo, Mhandisi David Munkyala, alisema mradi huo ni hatua muhimu katika kulinda rasilimali za maji na kurejesha ikolojia ya mito kwa manufaa ya wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























