Magazeti leo Desemba 31,2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha hakuna mtoto anayezuiwa kuanza au kuendelea na masomo kwa sababu ya kukosa sare, wakati shule zote nchini zikitarajiwa kufunguliwa rasmi Januari 13, 2025.

Prof. Shemdoe amesema kuwa agizo hilo linapaswa kusimamiwa kikamilifu katika maeneo yote ya nchi ili kuhakikisha kila mtoto anapokelewa shuleni bila masharti yanayokiuka miongozo na sera za elimu.

Amesisitiza kuwa mara mtoto anapopokelewa shuleni, masuala mengine ikiwemo sare, yataendelea kushughulikiwa akiwa tayari anaendelea na masomo, hatua itakayosaidia kuondoa vikwazo vinavyowafanya baadhi ya watoto kukosa haki yao ya msingi ya elimu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news