TRC yasitisha usafiri wa treni za SGR kati ya Morogoro na Dodoma

NA DIRAMAKINI

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limesitishwa safari za treni ya SGR kwa muda kuanzia tarehe 31 Disemba 2025 kati ya Morogoro-Dodoma na Dodoma-Morogoro kutokana na athari za mvua zilizopelekea uharibifu wa miundombinu katika eneo la Kidete (Kilosa, Morogoro) na Godegode (Mpwapwa,Dodoma).
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Desemba 31,2025 na Mkurugenzi Mkuu wa TRC,Mhandisi Machibya M. Shiwa

Kufuatia athari hiyo, safari zote za SGR zitakuwa kati ya Dar es Salaam-Morogoro na Morogoro-Dar es Salaam hadi pale marekebisho yatakapokamilika na usalama kuthibitishwa.

"Hivyo abiria wanashauriwa kubadili ratiba za safari zao kuendana na mabadiliko yaliyotokea. Shirika linaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza na watalaamu wanachukua hatua za haraka ili kurejesha huduma hizi."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here