Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amewasilisha ujumbe maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Sultan Haitham bin Tariq Al Said wa Oman. Akiwasilisha ujumbe wamejadili kuhusu masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Oman.


