Magazeti leo Januari 11,2026

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limefuta matokeo ya wanafunzi 89 waliohusika na udanganyifu na kuandika matusi katika karatasi zao wakati wa upimaji wa kitaifa wa darasa la nne na kidato cha pili.

Soma matokeo ya Kidato cha Pili na Darasa la Nne 2025 hapa》》》
Hayo yamebainishwa jijini Dar-es-Salaam Januari 10, 2026 na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani, Profesa Said Mohamed, wakati akitagaza matokeo ya kitaifa ya darasa la nne na kidato cha pili iliyofanyika Oktoba na Novemba 2025.

Soma matokeo ya Kidato cha Pili na Darasa la Nne 2025 hapa》》》
Amesema wanafunzi 41 walifanya udaganyifu na nane waliandika matusi kwenye skripti zao katika upimaji wa kitaifa wa darasa la nne huku wanafunzi 29 walifanya udaganyifu na 11 waliandika matusi kwenye skripti zao katika upimaji wa kitaifa wa kidato cha pili.

Soma matokeo ya Kidato cha Pili na Darasa la Nne 2025 hapa》》》

“Hatua hii imechukuliwa kwa mujibu wa Kifungu cha 5(2)(j) cha Sheria ya Baraza la Mitihani, Sura ya 107, kikisomwa pamoja na Kifungu cha 30(2)(b) cha Kanuni za Mitihani za mwaka 2016,” amesema Profesa Mohamed.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here