SERIKALI imekamilisha kufunga mifumo ya kunasa radi katika shule 12 zilizopo wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya kuwalinda wananchi pamoja na wanafunzi dhidi ya ajali za radi.
Hatua hiyo inakuja kufuatia mfululizo wa matukio ya radi wilayani humo ikiwemo tukio la Januari 27, 2025 lililopelekea vifo vya wanafunzi saba na kujeruhi 82 katika Shule ya Sekondari Businda.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Pasikasi Muragili ametoa taarifa hiyo katika mahojiano na waandishi wa habari na kueleza kuwa maboresho yanaendelea kabla ya shule kufunguliwa Januari 13, 2026.
Muragili amesema ili kufanikisha mpango huo serikali kupitia halmashauri hiyo imeweka mkakati wa kutenga fedha kidogo kidogo kila mwezi kwa ajili ya uwekaji wa mifumo ya kunasa radi.
Amesema mbali na maeneo ya shule serikali pia imeshatoa maelekezo kwa taasisi za umma na kijamii ikiwemo taasisi za kidini kuchukua hatua ya kuweka mifumo hiyo kwenye maeneo yao.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














