NA DIRAMAKINI
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Ladislaus Chang'a kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
Uteuzi wa Dkt.Chang'a umetangazwa leo Januari 29,2026 na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Moses Kusiluka kupitia taarifa kwa vyombo vya habari.Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Chang'a alikuwa akikaimu nafasi ya Ukurugenzi Mkuu wa TMA, baada ya kustaafu kwa Dkt. Agnes Kijazi aliyehudumu nafasi hiyo kwa karibu miaka 20.
Tags
Breaking News
Dr Samia Suluhu Hassan
Habari
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)
Tanzania Meteorological Agency (TMA)
Utabiri wa Hali ya Hewa Tanzania
Uteuzi
