Senegal yatwaa Ubingwa wa AFCON

NA DIRAMAKINI

TIMU ya Taifa ya Senegal imeibuka mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 leo Januari 18,2026 baada ya ushindi wa kishujaa katika mchezo wa fainali dhidi ya Morocco, ikithibitisha ubora na uimara wake katika soka barani Afrika.
Katika dimba la Prince Moulay Abdellah Stadium uliopo Rabat nchini Morocco, Papa Gueye dakika ya 94 aliiwezesha Senegal kuandikisha rekodi ya kipekee katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

Ushindi huo unaifanya Senegal kuendelea kujiimarisha kama moja ya mataifa yenye nguvu katika mchezo huo, huku kikosi chake kikionesha nidhamu, umoja na kiwango cha juu cha kiufundi katika mashindano yote.
Senegal ilitinga fainali baada ya ushindi wa 1–0 dhidi ya Misri katika nusu fainali, mchezo uliodumu hadi dakika za mwisho kabla ya Sadio Mané kupata bao la ushindi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here