Magazeti leo Januari 19,2026

Serikali imetoa onyo kwa waajiri na wafanyakazi wa sekta binafsi kuhakikisha kima cha chini cha mshahara kinatekelezwa ipasavyo.
Hayo yamebainishwa Januari 16, 2025 jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu wakati akitoa ufafanuzi kuhusu Amri ya Kima cha Chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi.

Mhe. Sangu amesema amri ya kima cha chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi imeanza kutumika kuanzia tarehe 1 Januari, 2026 na ilitangazwa kupitia Gazeti la Serikali la tarehe 13 Oktoba, 2025 ambapo kima cha chini cha Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 33.4.

Amesema, zoezi la mapitio ya kima cha chini cha Mshahara lilikuwa shirikishi ambapo Serikali kwa kushirikiana na Chama cha Waajiri na Vyama vya Wafanyakazi walikubaliana utekelezaji wake.

“Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi pamoja na Vyama vayo ili kuhakikisha mazingira ya kazi na hali za wafanyakazi zinaboreshwa ili kukuza tija na ustawi wa wafanayakazi,” amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here