ORAN-Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Iman Njalikai ameshiriki katika sherehe za uzinduzi wa Maonesho ya Saba (7) ya Kimataifa ya Chocolate na Kahawa (CHOCAF) yaliyofanyika jijini Oran Februari 4,2026.
Maonesho hayo yalijumuisha zaidi ya kampuni 100 zinazojihusisha na uchakataji wa kahawa na kakao kutoka ndani na nje ya Algeria na kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali pamoja na Mabalozi mbalimbali kutoka nchi zinazozalishaji kahawa kama vile Ethiopia, Uganda, Vietnam na Zimbabwe.
Mhe. Balozi Njalikai alitumia jukwaa hilo kukutana na wadau muhimu wa kahawa na kakao na kampuni za uchakataji wa kahawa na watengenezaji wa bidhaa zaKakao ambapo alielezea fursa zilizopo nchini katika uchakataji wa bidhaa hizo ambazo huzalishwa kwa wingi na kuwakaribisha kufanya biashara na Tanzania.
Aidha, Mhe. Balozi aliwaalika wafanyabiashara wa Algeria kuja nchini kushiriki Maonesho ya Kimataifa ya Dar es Salaam (7 7) ili kujionea fursa mbalimbali zilizopo na kutangaza biashara zao katika soko la Tanzania.



