Magazeti leo Februari 19,2026

Jeshi la Polisi mkoani Geita linamshikilia Bahati Bushirika anayetuhumiwa kujihusisha na wizi kwa kutumia dawa za kienyeji kuwafanya waathirika wapate usingizi ili kutekeleza uhalifu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SCAP) Safia Jongo ametoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari na kueleza mhusika ni mkazi wa kata ya Nyankumbu.

Amesema uchunguzi umebaini mtuhumiwa alijiingiza kwenye matukio ya uhalifu baada ya kuacha uganga wa tiba za asili kwa madai ya kukosa wateja pamoja na kukiuka masharti ya kazi hiyo.

Amesema mtuhumiwa anadaiwa kutumia dawa za asili kuwafanya waathirika wapate usingizi kabla ya kutenda uhalifu ambapo alikamatwa katika oparesheni ya mwezi Februari 2026.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here