REA yatoa elimu ya umeme mkoani Tanga

PANGANI-Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea na zoezi la uhamasishaji wananchi kujiunga na huduma ya umeme.
Uhamasihaji umefanyika wilayani Pangani ambapo maafisa wa REA na TANESCO wametembelea nyumba ambazo zimenufaika na miradi ya umeme pamoja na kufanya mikutano ya hadhara yenye lengo kuu la kuwapa uelewa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na huduma ya umeme.

Akizungumza wakati wa uhamasishaji Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka REA, ndugu Abdulrazack Mkomi amesema,kwa sasa taratibu za uombaji huduma ya umeme zimeboreshwa zaidi na hakuna tena mambo ya kutumia fomu kufanya maombi.
Mkomi amesema, kwa kutumia tu namba ya kitambulisho cha Taifa (NIDA) mwananchi anaweza kufanya ombi la umeme moja kwa moja TANESCO kupitia huduma ya NIKONEKT.

“Kwa kutumia simu janja, mwananchi atapakua huduma ya Nikonekt na kufanya maombi au kama ni simu ya kawaida atabonyeza *152*00# na kisha kufuata maelekezo ya kufanya ombi, hakuna mawakala wanaosajili maombi mtaani tafadhali tuepuke vishoka,” Mkomi amesisitiza.
Aidha,Mkomi ameongezea kuwa, pamoja na umeme kufika majumbani ni vyema wananchi waliopo eneo la mradi wakachangamkia na kutumia fursa hiyo kujiunga mapema na huduma ya umeme.

Aidha, wananchi wameombwa kuendelea kutunza miundombinu ya umeme kwani mpaka umeme unafikishwa katika kijiji au kitongoji umesafiri kutoka umbali mrefu na umepita katika njia salama ndio maana unawaka, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kulinda na kutunza miundombinu ya umeme ili kuhakikisha usalama muda wote.

Halikadhalika, uelimishaji huu utaendelea wilaya kwa wilaya, Kata kwa kata kijiji kwa kijiji na kitongoji kwa kitongoji mkoani Tanga.
Vilevile, REA itaendelea kutekeleza na kusimamia miradi tofauti tofauti ya umeme ikiwemo miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji na na miradi ya ujazili ili kuhakikisha kila mwananchi wa mkoa wa Tanga hususani mwananchi aishie kijijini na pembezoni mwa jiji anafikiwa na huduma ya umeme.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here