Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa, amesema kuwa ndani ya siku 100 za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan,sekta ya uchukuzi imepata mafanikio makubwa yaliyoimarisha reli, bandari, usafiri wa majini na anga, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.
Ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Februari 1, 2026 katika Ukumbi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo jijini Dodoma, katika kutoa taarifa ya utekelezaji wa ahadi za Rais samia ndani ya siku 100.
Aidha, amebainisha kuwa Serikali imefufua na kuboresha Reli ya TAZARA, hatua itakayoongeza uwezo wa reli hiyo na kuimarisha biashara na nchi za Kusini mwa Afrika.

Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo





















