Magazeti leo Februari 24,2026

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk. Juma Zuberi Homera, amewasili mjini Geneva, nchini Uswisi kuhudhuria Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa unaoanza tarehe 23 Februari 2026.Katika mkutano huo wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Mhe. Waziri anatarajiwa kuwasilisha taarifa ya nchi kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Tanzania.

Awali, Homera alitembelea Ofisi za Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania mjini Geneva, ambako alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi Dk. Abdallah Possi, ambaye ni Mwakilishi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ofisi za Umoja wa Mataifa, pamoja na Balozi na Naibu Mwakilishi wa Kudumu Dk. Hoyce Temu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here