Magazeti leo Februari 7,2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Morogoro imewataka walipakodi na wafanyabiashara wa Mkoa wa Morogoro kuanza kuuzoea na kuutumia Mfumo Mpya wa Usimamizi wa Kodi za Ndani wa Kielektroniki (IDRAS), unaolenga kuboresha ukusanyaji na usimamizi wa kodi kwa njia ya kisasa, rahisi na yenye ufanisi zaidi.
Akizungumza na walipakodi na wadau wa kodi mkoani humo Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka TRA makao makuu Bw. Ernest Shirima, amesema mfumo wa IDRAS unakwenda kuchukua nafasi ya mifumo mbalimbali inayotumika kwa sasa ndani ya TRA, hatua itakayowezesha kuimarisha utoaji wa huduma za kodi kwa njia ya kidijitali.

Bw. Shirima amesema kuwa utekelezaji wa IDRAS utaleta mapinduzi makubwa kwa kuondoa matumizi ya huduma za makaratasi (manual) na kuwezesha shughuli zote zinazohusiana na usimamizi wa kodi za ndani kufanyika kwa njia ya kielektroniki.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here