NA DIRAMAKINI
MSIMAMO wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kwa msimu wa 2025/2026 unaendelea kuonesha ushindani mkubwa huku timu mbalimbali zikiendelea kupambana kuwania nafasi za juu pamoja na kuepuka kushuka daraja.
Klabu ya JKT Tanzania inaongoza ligi kwa pointi 24 baada ya kucheza mechi 14, ikishinda michezo sita, kutoka sare sita na kupoteza michezo miwili. JKT Tanzania imefunga mabao 16 na kuruhusu mabao tisa.
Nafasi ya pili inashikiliwa na Young Africans SC yenye pointi 22 baada ya kucheza mechi nane, ikishinda michezo saba na kutoka sare moja bila kupoteza mchezo wowote. Young Africans SC imefunga mabao 21 na kuruhusu mabao mawili pekee.
Mtibwa Sugar ipo nafasi ya tatu kwa pointi 21 ikifuatiwa na Pamba Jiji na Namungo FC zinazoshika nafasi ya nne na tano kwa pointi 20 kila moja.
Mabingwa watetezi Simba SC wapo nafasi ya sita wakiwa na pointi 16 baada ya kucheza mechi saba, huku Azam FC ikishika nafasi ya saba pia ikiwa na pointi 16 baada ya mechi nane.

