Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni kuimarisha ucha Mungu na mshikamano-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewataka Waislamu na wananchi wote kuutumia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuimarisha uchamungu, mshikamano wa kijamii na kudumisha amani na utulivu nchini.
Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza kuendelezwa kwa mafunzo ya dini, kusaidiana na kutoa sadaka kwa wahitaji, pamoja na kuhimiza wafanyabiashara kutopandisha bei za bidhaa muhimu katika kipindi hiki.

Aidha, ameeleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa muhimu na kuvitaka vyombo husika kusimamia mwenendo wa bei na usafi wa mazingira wakati wa Ramadhani.

Rais Dkt. Mwinyi amewaomba wananchi kuendelea kuishi kwa amani, kuheshimiana na kuzingatia sheria, huku akimuomba Mwenyezi Mungu awajaalie Waislamu wote kutekeleza ibada ya saumu kwa ikhlasi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here