DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemwapisha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, atakayekuwa anashughulikia masuala ya Utawala (Huduma za Hazina), Bw. Nsubili Joshua, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Uapisho huo umeshuhudiwa na Viongozi wa Wizara ya Fedha, wakiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), Kaimu Katibu Mkuu, Bw. Elijah Mwandumbya, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Lusius Mwenda, na Maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha.
Bw. Nsubuli Joshua, anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu-Huduma za Hazina, Bi. Jenifa Omolo, ambaye aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa Katibu Mkuu wa Wizara mpya ya Vijana.




