Serikali kuchukua hatua za kinidhamu kwa waajiri wote wasiozingatia sheria

NA ANTONIA MBWAMBO

“Ninatoa rai kwa kwa Waajiri wote, Mamlaka za ajira na Mamlaka za nidhamu kuwasilisha vielelezo vya rufaa na malalamiko Tume ya Utumishi wa Umma kwa wakati kama Sheria inavyoelekeza vingenevyo Serikali haitasita kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yao”.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete, akizungumza na Maafisa Utawala na Maafisa Sheria (hawapo pichani) wakati akifungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi kilichofanyika katika ukumbi wa NSSF Mkoani Morogoro leo tarehe 9 February, 2026.

Rai hiyo imetolelewa leo tarehe 9 Februari, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha Tume ya Utumishi wa Umma na Mamlaka za Maji nchini kuhusu utekelezaji wa sheria ya utumishi wa umma Sura 298 na matumizi ya mfumo wa kielektroni wa kushughulikia rufaa na malalamiko na uwasilishaji wa taarifa za kiutumishi tume.
Mhe. Kikwete alisema kuwa Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za Nidhamu katika Utumishi wa Umma zinaweza kuwasilisha vielelezo vya rufaa na malalamiko ya watumishi wao Tume kupitia Mfumo wa Kielektroni wa Kushughulikia Rufaa na Malalamiko katika Utumishi wa Umma na Uwasilishaji wa Taarifa za Kiutumishi (PSCMIS).

“Ninafahamu kuwa wapo Waajiri, Mamlaka za Ajira na Mamlaka za Nidhamu ambazo hazitekelezi wajibu wao ipasavyo hasa Tume inapowaelekeza kuwasilisha vielelezo vya rufaa na malalamiko, jambo hili limekuwa likisababisha watumishi wa Umma kukaa muda mrefu bila kupata haki zao na Serikali kupata hasara,” alisema Mhe. Kikwete.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe. Hamisa Kalombola, wakati wa kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026.

Aliongeza kuwa, muda wa kuwasilisha vielelezo hivyo unapopita, Tume hulazimika kuamua rufaa hizo kwa kutumia vielelezo vya upande mmoja kwa kuzingatia sheria, jambo hili siyo sawa kwa kuwa Mamlaka haziwatendei haki Warufani na Walalamikaji pamoja na Serikali iliyowaamini na kuwapa dhamana ya kusimamia Utumishi wa Umma.

Kwa kuzingatia utawala bora unaoshamilishwa na uwepo wa mifumo ya TEHAMA, Warufani wataweza kufuatilia, kufahamu hali ya rufaa na malalamiko yao yamefikia hatua gani kwa urahisi.
Viongozi wa Tume ya Utumishi wa Umma wakimsubiri Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete kuwasili katika katika kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026.
Washiriki wa kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipokuwa akizungumza nao leo Mkoani Morogoro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Umma baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Sekretarieti ya Tume ya Utumishi wa Umma baada ya Waziri huyo kufungua kikao kazi cha mafunzo ya Tume ya Utumishi wa Umma kwa Mamlaka za Maji Tanzania cha Utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma na Matumizi ya Mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia Rufaa na uwasilishwaji wa taarifa za masuala ya kiutumishi leo tarehe 9 Februari, 2026.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala tumepewa dhamana ya kuhakikisha dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kujenga Utumishi wa Umma wenye uadilifu na unaowajibika kwa wananchi kwa kutoa huduma bora inatimia kupitia Tume ya Utumishi wa Umma" Mhe. Kikwete alisisitiza.

Vile vile, aliwashukuru Wanahabari kwa kuhabarisha umma kuhusu jitihada zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuijenga Tanzania hasa katika kuboresha haki za Watumishi wa Umma na kuimarisha Utawala Bora.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here