MWANZA-Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza imefanikiwa kudhibiti fedha kiasi cha Shilingi millioni 85,006,000, fedha ambayo ni madai ya walimu wa shule za sekondari katika Halmashauri ya jiji la Mwanza, madai ambayo yalicheleweshwa kwa zaidi ya miezi sita.
Hayo yamesemwa leo Februari 25,2026 na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza Mha.Abnery Mganga alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kwa lengo la kutoa taarifa kwa umma.
Mafanikio haya ni baada ya TAKUKURU kufanya Uchambuzi wa mfumo na Halmashauri kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa na TAKUKURU ambapo imepelekea walimu hao 77 kulipwa stahiki zao.
