DODOMA-Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inatarajia kuzindua Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya mwaka 2025, kupitia Wizara ya Fedha.
Sera hiyo inalenga kuimarisha ufanisi, uwazi na uwajibikaji katika matumizi ya rasilimali za umma, pamoja na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi na makundi maalum ya kijamii katika shughuli za ugavi.
Uzinduzi rasmi wa sera hiyo unatarajiwa kufanyika Aprili 8, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
.jpg)