Kamati ya Bunge yashuhudia maendeleo ya ujenzi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali jijini Mwanza

MWANZA-Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imefanya ziara ya kutembelea na kukagua Jengo la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lililopo Buswelu jijini Mwanza.
Kamati hiyo iliyoko chini ya Mwenyekiti wake, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) imefanya ziara hiyo tarehe 16 Machi, 2026 na kwa lengo la kuona Maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, ambapo kukamilika kwake kutarahisisha upatikanaji wa Huduma za Kisheria kwa Wananchi.

Sambamba na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, pia jengo hilo linatarajiwa kutumiwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.
Aidha, Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika mkoa wa Mwanza unajengwa na Mkandarasi Suma JKT na kusimamiwa na mshauri wa majengo TBA na umefikia asilimia 74.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here