Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba, ameaga rasmi baada ya kuhudumu kwa miaka 10 mfululizo tangu kuteuliwa mwaka 2016 na Rais Dk. John Magufuli.
Rioba amesema, kipindi chake kilikuwa na changamoto kubwa, akibainisha kuwa alipitia “vita ngumu” lakini aliendelea kuhudumu hadi kuongezewa muda wa uongozi mwaka 2024 na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.
Ametoa shukrani kwa viongozi mbalimbali wa serikali, wafanyakazi wa TBC na Watanzania kwa ushirikiano waliompa katika kipindi chote cha uongozi wake.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo













