Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuimarisha malezi na makuzi ya watoto, kuwawezesha wanawake na vijana kiuchumi pamoja na kujenga familia imara, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuharakisha maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.
Ameyasema hayo Julai 4, 2026 wakati akifungua Kongamano la Usiku wa Mtoko wa Familia lililoandaliwa na Rizex for Life Foundation katika Ukumbi wa Bombambili, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, ambapo pamoja na kutoa elimu ya malezi na makuzi ya watoto, taasisi hiyo imefadhili vijana 10, wakiwemo wasichana watano na wavulana watano, kujiunga na masomo ya ufundi stadi katika Chuo cha VETA.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























