Serikali imeanza kuimarisha usimamizi wa huduma za macho kwa lengo la kulinda afya ya wananchi dhidi ya madhara yatokanayo na matumizi yasiyo sahihi ya miwani pamoja na huduma zisizoidhinishwa.
Hatua hiyo imeelezwa na Msajili wa Baraza la Optometria, Bw. Sebastiano Millanzi, alipokuwa akiongoza zoezi la usimamizi shirikishi katika vituo vinavyotoa huduma za optometria kwa wilaya za Temeke na Ubungo, jijini Dar es Salaam kwa ushirikiana na timu kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu wa mkoa pamoja na Manispaa ya Temeke.






































Amesema lengo la zoezi hilo ni kutoa elimu kwa wafanyabiashara wanaouza miwani na kuwajengea uelewa wananchi kuhusu matumizi sahihi ya miwani, pamoja na umuhimu wa kupata huduma za macho kutoka kwa wataalamu waliothibitishwa.
Bw. Millanzi amebainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara wamekutwa wakitoa huduma bila usajili, hali inayoweza kuhatarisha afya za watumiaji wa huduma hizo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo









