Rais Dkt.Mwinyi aishukuru Oman kwa kuendelea kuwa mshirika muhimu wa maendeleo Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru Serikali ya Oman kwa kuendelea kutoa misaada inayochangia maendeleo ya Zanzibar katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, utalii, utamaduni na uhifadhi wa urithi wa Mji Mkongwe.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Machi 10, 2026, aliposhiriki futari iliyoandaliwa na Balozi Mdogo wa Oman Zanzibar, Balozi Said Salim Al-Sinawiy, katika Hoteli ya Golden Tulip, Airport, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Amesema, Oman imeendelea kuwa na uhusiano wa kihistoria na kidugu na Zanzibar na kuahidi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuimarisha ushirikiano huo.

Kwa upande wake, Balozi Said Salim Al-Sinawiy amemhakikishia Rais Dkt. Mwinyi kuwa Oman itaendelea kuwa mshirika muhimu wa maendeleo ya Zanzibar, hususan katika sekta za utalii, elimu, uchumi wa buluu pamoja na utamaduni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here