Rais Dkt.Mwinyi atoa salamu za pole kifo cha Waziri Lukuvi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi ametuma salamu za pole kufuatia kifo cha Mbunge wa Jimbo la Ismani na aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. William Vangimembe Lukuvi (Mb.).

Katika salamu zake alizozitoa leo Machi 25, 2026, Rais Dkt. Mwinyi amesema, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo hicho, akieleza kuwa Taifa limepoteza kiongozi shupavu aliyetoa mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi.

Ameeleza kuwa, marehemu Lukuvi atakumbukwa kwa uongozi wake thabiti, uzalendo uliotukuka na kujitolea kwake kwa muda mrefu katika kulitumikia Taifa katika nyadhifa mbalimbali za uongozi.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ametoa pole za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, familia ya marehemu, ndugu, jamaa pamoja na Watanzania wote kwa msiba huo mzito.
"Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa kwa Taifa, uongozi wake thabiti na uzalendo wake uliotukuka katika kulitumikia Taifa kwa muda mrefu. Ninatoa pole za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na Watanzania wote kwa msiba huu mzito. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina."

Rais Dkt.Mwinyi amemuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na kuwapa faraja na subira wafiwa wote katika kipindi hiki kigumu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here