DODOMA-Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Fedha, Bw. Benny Mwaipaja amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kutoka Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Bw.Titus Kaguo, baada ya kumtembelea katika ofisi zake zilizopo Wizara ya Fedha (Treasury Square) jijini Dodoma.
Katika kikao hicho, viongozi hao walijadili masuala mbalimbali yanayohusu uratibu na uimarishaji wa mawasiliano ya Serikali kwa lengo la kuhakikisha taarifa muhimu za maendeleo ya taifa zinawafikia wananchi na wadau kwa ufanisi.Aidha, mazungumzo yao yalijikita katika kupanga mikakati ya ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili ili kuimarisha utoaji wa taarifa sahihi kuhusu utekelezaji wa Ajenda ya Kitaifa ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.
