Waziri Balozi Kombo apokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Kenya

DAR-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amepokea rasmi nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Kenya nchini Tanzania, Mhe. Catherine Karemu leo Machi 3, 2026.
Mheshimiwa Kombo amempongeza Balozi Karemu kwa uteuzi wake na kueleza kuwa, wizara itaendelea kushirikiana kwa karibu na Ubalozi wa Kenya katika kipindi chake cha uwakilishi. Vilevile, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo.
Katika mazungumzo yao, viongozi hao wamejadili maeneo mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya, ikiwemo jitihada za kuondoa vikwazo vya kibiashara (NTBs) ili kurahisisha biashara kati ya raia wa nchi hizo jirani.

Aidha, wameangazia hatua za kuongeza thamani ya mazao ya biashara ndani ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa manufaa ya uchumi wa kikanda.
Mazungumzo hayo pia yamegusia maandalizi yanayoendelea ya Kikao cha Wakuu wa Nchi wa EAC kinachotarajiwa kufanyika Machi 7, jijini Arusha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here