DAR-Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, na Rais mstaafu wa Malawi,Dkt. Lazarus Chakwera, amekutana na kufanya Mazungumzo na Tume ya uchunguzi wa Matukio ya vurugu za Uchaguzi na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29,2025.
Ujumbe huo wa Jumuiya ya Madola umekutana na Tume hiyo katika ofisi zao zilizopo jijini Dar es Salaam mapema hii leo.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Othuman Chande amesema, mazungumzo yao yalijikita zaidi kueleza shughuli za tume hiyo na Hadidu za rejea za tume.
Chakwera anaendelea na ziara yake ya kikazi ambayo anatarajia kuhitimisha Aprili 16,mwaka huu.
