DAR-Mwenyekiti wa Chama cha ADC,Hamad Rashid amesema kuwa,Tume ya Uchunguzi imefanya kazi nzuri ya kuleta ripoti ambayo imeonesha wapi kama taifa lilikosea na namna gani ya kusonga mbele kwa sasa.
Hamad Rashid amesema hayo wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam ambapo amesema,ripoti hiyo ni hatua muhimu katika kuelekea maridhiano na kila mwenye nia njema na Taifa basi ataondoa tofauti aliyonayo na kujikita katika kutafuta suluhu na kujenga umoja wa kitaifa.