Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kwa kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Watoto Ulimwenguni (UNICEF) inatoa mafunzo maalum kwa Maafisa Ustawi na Maafisa Lishe wa ngazi ya mkoa na halmashauri kutoka mikoa ya Dodoma na Dar es salam, ili kuwajengea uwezo wa kuandaa vifaa vya kujifunzia na kuchezea watoto kwenye vituo vya kulelea watoto wadogo mchana vilivyopo masokoni.

Mafunzo hayo kwa maafisa hao yameanza kutolewa Aprili 13, 2026 mkoani Morogoro, kwa lengo la kuwajengea uwezo utakaoimarisha ubora wa malezi na ujifunzaji kwa watoto wadogo katika ngazi za mikoa na halmashauri.
Akizungumzia mafunzo hayo, Mratibu wa Mafunzo hayo kutoka OWM – TAMISEMI Bi Amina Mfaki amesema kuwa washiriki watapatiwa ujuzi wa kuandaa vifaa vya kujifunzia na kuchezea kwa kutumia rasilimali zinazopatikana katika mazingira yao, hatua inayotarajiwa kuongeza ubunifu, kupunguza gharama na kuhakikisha upatikanaji wa vifaa rafiki kwa watoto katika vituo hivyo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























