Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga limeendelea kudhibiti vitendo vya uhalifu, baada ya kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 200 katika operesheni maalumu zilizofanyika kuanzia Juni 1 hadi Julai 16, 2026.












Akizungumza Julai 17, 2026 Tanga, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi, amesema kuwa Katika kipindi hicho cha wiki sita, jeshi hilo limebainisha kuwa hali ya ulinzi na usalama mkoani hapa ni shwari, huku likisisitiza kuwa mafanikio hayo yanatokana na ushirikiano kati ya polisi na wananchi kupitia falsafa ya polisi jamii.Katika hatua inayoashiria mwendelezo wa mapambano dhidi ya ukatili na uhalifu uliokithiri Kamanda huyo alisema kuwa jumla ya watuhumiwa 51 walitiwa hatiani na kuhukumiwa vifungo mbalimbali jela baada ya upelelezi wa kesi zao kukamilika.
Aliwajaka waliopewa adhabu kali ni Sadiki Waziri, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kusafirisha dawa za kulevya huku adhabu kama hiyo ya miaka 30 pia imewakuta Julius Mustafa (kwa kosa la kulawiti) na Kilimo Issaya (kwa kosa la kuzini na maharimu).
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo










