Magazeti leo Aprili 17,2026

Watoto 30 kati ya zaidi ya 800 wamejiunga na programu maalum ya Soccer School inayoendeshwa na GSM Foundation, yenye lengo la kukuza na kuendeleza vipaji vya soka kwa vijana.
Akizungumza na waandishi wa habari, Rais wa Klabu ya Yanga, Hersi Said amesema mafunzo hayo yatawasaidia watoto kujijengea misingi bora ya soka ikiwemo nidhamu, ujuzi na ushindani, hatua itakayowawezesha kufikia ndoto zao za kucheza katika klabu kubwa ndani na nje ya nchi.

Amesema programu hiyo ni sehemu ya jitihada za kuinua vipaji vya soka nchini na kutoa fursa kwa vijana kuonesha uwezo wao mapema.

Aidha, Hersi amesema pia kuna fursa kwa watoto wengine kujiunga na mafunzo hayo kwa kuchangia gharama nafuu, huku akibainisha kuwa vituo vya mafunzo vitafunguliwa katika maeneo mbalimbali nchini ili kuwafikia vijana wengi zaidi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here