WASHINGTON D.C-Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo anayesimamia Idara ya Afrika, Bw. Abebe Selassie, katika Ofisi za makao makuu ya IMF, jijini Washington D.C Nchini Marekani, pembezoni mwa Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayofanyika, Jijini humo, ambapo walijadiliana masuala mbalimbali yanayohusu uchumi wa Tanzania
Mhe. Balozi Omar, alieleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali kusimamia uchumi wake unaoendelea kukua lakini pia inachukua hatua mbalimbali madhubuti za kuhakikisha kuwa uchumi unaendelea kuwa imara licha ya misukosuko hiyo
Mikutano hiyo ya uwili (bilateral meetings), imewashirikisha pia Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Dkt. Elsie Kanza, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi, Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, Msaidizi wa Katibu wa Baraza la Mawaziri, Bw. Francis Mossongo na maafisa wengine wa Serikali.
Tags
Habari
International Monetary Fund (IMF)
Kimataifa
Mikutano ya Kipupwe ya IMF
Wizara ya Fedha Tanzania



