DAR-Aliyekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha NLD,Doyo Hassan Doyo amesema, ana matumaini makubwa na Tume ya Jaji Chande inayochunguza Matukio ya Vurugu wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29,2025.
Imani na matumaini ya Doyo kwa tume hiyo yanatokana na ukweli kwamba, tume imesheheni watu muhimu wenye ubobevu na weledi mkubwa kama vile Majaji Wastaafu, Mawaziri Wastaafu na Viongozi wakubwa wa Ulinzi na Usalama Wastaafu, na hivyo Watanzania watarajie ripoti itakayokidhi matarajio yao.
.jpeg)