Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yashiriki kikamilifu Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka 2026

NJOMBE-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeshiriki kikamilifu Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kitaifa katika viwanja vya Lunyanywi mkoani Njombe, ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Katika tukio hilo, mshindi wa Tuzo ya Mfanyakazi Bora wa Benki Kuu, Bw. Rweyemamu Barongo, alipokea hati ya kutambua mchango wake iliyotolewa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA). 

Hati hiyo inaakisi juhudi na weledi wa watumishi wa Benki Kuu katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Sambamba na maadhimisho ya kitaifa, Benki Kuu ya Tanzania ilishiriki pia katika maadhimisho yaliyofanyika katika kanda mbalimbali nchini kupitia ofisi zake zilizopo Dodoma, Dar es Salaam, Zanzibar, Arusha, Mwanza na Mtwara, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kuenzi mchango wa wafanyakazi kote nchini.
Maadhimisho ya mwaka 2026 yaliongozwa na kaulimbiu “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here