NA DIRAMAKINI
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa leseni ya kibenki kwa Radiance Microfinance Bank Limited,hivyo kuiruhusu kuanza kutoa huduma za kibenki kama benki ya huduma ndogo za fedha nchini.
Kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa leo Mei 22,2026 na Naibu Gavana anayeshughulikia Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha,Sauda K. Msemo,BoT imesema leseni hiyo ilianza kutumika rasmi Mei 4.2026.
Makao makuu ya benki hiyo yatakuwa katika Kiwanja Na.16/1, Elia Complex katika makutano ya Mtaa wa Zanaki na Barabara ya Bibi Titi jijini Dar es Salaam.
Benki Kuu ya Tanzania imeeleza kuwa,hatua hiyo ni sehemu ya wajibu wake wa kusimamia na kudhibiti taasisi za kifedha nchini.
Mwaka huu Benki Kuu ya Tanzania inaadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1966.
.jpeg)
