Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Karibu-Kilifair 2026 yanatarajiwa kufanyika kwa siku nne mfululizo jijini Arusha kuanzia Juni 4, 2026, huku zaidi ya nchi 14 kutoka mataifa mbalimbali zikitarajiwa kushiriki.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mkurugenzi wa Kilifair Promotion Co. Ltd, Tom Kunkler amesema maonesho hayo ya mwaka huu yamejikita zaidi katika ubunifu na utoaji wa fursa kwa wadau wa utalii wa ndani na nje ya nchi.Amesema Tanzania imeendelea kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa utalii wa mikutano na biashara kutokana na mazingira ya kipekee yanayounganisha shughuli za biashara na vivutio vya asili.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


















