Nidhamu na uadilifu ni msingi wa maendeleo ya Taifa-Waziri Ridhiwani Kikwete

DAR-Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete amewataka viongozi wanaochipukia nchini kutumia elimu na mafunzo ya uongozi waliyoipata kwa manufaa ya taifa na jamii kwa ujumla.
Waziri Kikwete ametoa kauli hiyo leo Mei 15, 2026 aliposhiriki Mahafali ya Tisa ya Wahitimu wa Kozi za Uongozi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, ambapo pia aligawa vyeti kwa wahitimu wa programu mbalimbali za uongozi.
Kozi hizo zimehusisha mafunzo ya Wanawake Viongozi, Viongozi Wanaochipukia pamoja na kozi za uongozi katika madaraja tofauti kwa lengo la kukuza uwezo wa viongozi katika taasisi za umma na binafsi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Kikwete amesema,nidhamu na uadilifu ni msingi muhimu wa maendeleo ya taifa na kwamba viongozi wakizingatia maadili hayo wataweza kuleta mabadiliko chanya nchini na barani Afrika kwa ujumla.
“Nidhamu na uadilifu vikizingatiwa ipasavyo vitaweza kuiponya Tanzania na Afrika kwa ujumla,” amesema Waziri Kikwete.

Aidha, amesema kozi hizo zinazoendeshwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Vyuo vya Aalto cha Finland na Yale cha Marekani zina mchango mkubwa katika kuandaa kizazi cha viongozi wenye uwezo, weledi na maadili ya uongozi bora.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here