Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi amewataka Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu serikalini kushiriki wenyewe kikao kazi cha kitaifa kitakachofanyika jijini Dodoma Juni 1 hadi 3, 2026 ili kupata maelekezo mahsusi ya usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Bw. Mkomi amesema kikao hicho kitawakutanisha Wakurugenzi na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa lengo la kujadili namna bora ya kuongeza ufanisi, uwajibikaji na usimamizi wa watumishi wa umma.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo







