Magazeti leo Mei 28,2026

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Juma Mkomi amewataka Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu serikalini kushiriki wenyewe kikao kazi cha kitaifa kitakachofanyika jijini Dodoma Juni 1 hadi 3, 2026 ili kupata maelekezo mahsusi ya usimamizi wa rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Bw. Mkomi amesema kikao hicho kitawakutanisha Wakurugenzi na Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu kutoka Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa lengo la kujadili namna bora ya kuongeza ufanisi, uwajibikaji na usimamizi wa watumishi wa umma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here