DAR-Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu,Dkt. Jim Yonazi pamoja na Mwenyekiti mwenza,Dkt.Islam Seif Salum Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar wameongoza kikao cha Makatibu Wakuu kwa ajili ya maandalizi ya Kikao cha Ushirikiano cha Ngazi ya Mawaziri.

Lengo kuu la vikao vya ushirikiano kwa pande hizi mbili za Muungano ni kubadilishana uzoefu katika Sekta mbalimbali ili kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya kila siku Serikalini.
Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mtaa wa Magogoni jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei,2026.
Tags
Dr Jim Yonazi
Habari
Makatibu Wakuu
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar



















