Rais Dkt.Samia ateua,atengua na kufanya uhamisho wa viongozi

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi na uhamisho wa viongozi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt.Moses Kusiluka,Rais Dkt.Samia amemteua Dkt.Eveline Munisi kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, akichukua nafasi ya Rahma Riyadh Kisuo, ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Pia, Eliakim Maswi amehamishwa kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, kwenda kuwa Katibu Muuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalumu.

Aidha,Dkt.John Jingu amehamishwa kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalumu kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here