NA DIRAMAKINI
RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini Tanzania kesho Mei 3,2026 ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano wa pande mbili.
Kwa mujibu wa taarifa ya Serikali, Rais Kagame atapokelewa na mwenyeji wake, Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, na kufanya mazungumzo rasmi yatakayolenga kukuza ushirikiano wa kiuchumi na kidiplomasia.
Tanzania na Rwanda zimeendelea kuimarisha mahusiano kupitia biashara na uwekezaji, huku Tume ya Pamoja (JPC) ikitumika kusimamia ushirikiano katika sekta mbalimbali.
Ziara hiyo inatarajiwa kuongeza kasi ya ushirikiano wa kikanda katika sekta za kimkakati.
