Wizara ya Fedha na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Na. 686 la Desemba 19, 2025 pamoja na Muundo na Mgawanyo wa Majukumu ya Wizara ulioidhinishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Machi 12, 2026.
Majukumu ya msingi ya Wizara ni pamoja na:
kubuni na kusimamia utekelezaji wa sera za uchumi jumla, fedha, ununuzi wa umma na ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi;kuandaa na kusimamia utekelezaji wa miongozo ya usimamizi wa bajeti ya Serikali; kusimamia uchumi; kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali; kusimamia na kuratibu upatikanaji wa fedha za nje na kuimarisha mahusiano na taasisi za fedha za kikanda na kimataifa.