Wadau wa maendeleo wameitaka Serikali kuhakikisha Bajeti ya Taifa ya mwaka 2026/2027 inatekelezwa kwa kuzingatia usawa wa kijinsia ili kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Kuli hiyo ilitolewa jana katika mjadala wa uchambuzi wa Bajeti ya Taifa ulioandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kupitia jukwaa la Kijiwe cha Kahawa, lililowakutanisha wadau wa maendeleo, wanaharakati, wataalamu wa uchumi na viongozi wa serikali za mitaa.
Mratibu wa TGNP, Anna Sangai, alisema bajeti yenye mrengo wa kijinsia ni muhimu katika kuhakikisha wanawake, vijana, watoto na makundi mengine yaliyo pembezoni yanapata fursa sawa za maendeleo na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa taifa.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo





















