SONGWE-Muonekano wa juu wa Bwawa la Umwagiliaji la Itumpi lililojengwa kwa ufadhili wa Shirika la KOICA chini ya usimamizi wa Shirika la GOOD NEIGHBORS. Bwawa hilo limezinduliwa rasmi Mei 28,2026 na Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Jabiri Makame.
Mradi huo wa kimkakati umegharimu jumla ya shilingi milioni 510, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imechangia asilimia 20 ya gharama zote za ujenzi. Bwawa hilo linatarajiwa kuongeza tija katika shughuli za kilimo cha kahawa cha umwagiliaji, kuimarisha usalama wa chakula, pamoja na kuinua uchumi wa wananchi wa eneo la Itumpi na maeneo jirani.


