ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi amejumuika na viongozi mbalimbali, wanafamilia na wananchi katika Sala ya Jeneza kumsalia marehemu Furtuna Saleh Mbamba, katika Msikiti wa Jamiu Zinjibar, Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Marehemu Furtuna Saleh Mbamba alifariki dunia tarehe 24 Juni 2026 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Al Rahma, Kilimani. Marehemu alikuwa mke wa kwanza wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad. Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema Peponi. Amin.





